z-logo
open-access-imgOpen Access
Mnyambuliko wa Vitenzi Katika Lugha za Kiafrika: Mfano katika Lugha ya Kimasaaba Nchini Uganda
Author(s) -
Willy Wanyenya
Publication year - 2020
Publication title -
east african journal of swahili studies
Language(s) - Slovenian
Resource type - Journals
eISSN - 2707-3475
pISSN - 2707-3467
DOI - 10.37284/eajss.2.2.184
Subject(s) - humanities , physics , art
Katika makala hii, mtafiti anaeleza jinsi vitenzi vya lugha za Kiafrika vinavyonyambuliwa na kuleta maana tofauti tofauti. Anafanya hivyo kwa kurejelea Kimasaaba ambayo ni lugha inayozungumzwa na Wamasaaba nchini Uganda. Unyambuaji wa vitenzi ni jambo la kawaida na huwa linatekelezwa katika lugha mbalimbali. Hivyo basi, katika makala hii, mtafiti anaeleza mnyambuliko ya vitenzi katika lugha ya Kimasaaba. Anawasilisha mkusanyiko wa vitenzi na kueleza jinsi vinavyonyambuliwa na wazungumzaji. Aidha, mtafiti anaeleza namna vitenzi hivyo vinatumiwa katika sentensi. Mtafiti anafanya hivi kwa sababu lugha nyingi za Kiafrika hazijatafitiwa na kuna mambo mengi sana mazuri ambayo hayajulikani kwa ulimwengu. Katika kazi hii, mtafiti anaandika vitenzi mbalimbali katika lugha asili halafu anavitafsiri katika Kiswahili. Kwenye kazi hii, madhumuni ya utafiti ni kudhihirisha utaratibu wa kunyambua vitenzi katika Kimasaaba. Pili, kueleza maana tofauti zinazotokana na mnyambuliko ya vitenzi. Tatu, kuonyesha kuwa Kimasaaba ni lugha inayoendelea kukua kama lugha zingine za Kiafrika. Mkabala wa utafiti ulikuwa wa nyanjani. Kwa kutumia mkabala huu, mtafiti alizuru nyanjani ambako aliendeleza mahojiano na wahojiwa wake. Majibu ya wahojiwa yalijumlisha data ambazo zilihitajika na mtafiti. Mwishowe, matokeo ya utafiti huu yanaonyesha kuwa Kimasaaba kama lugha nyingine za Kiafrika ina vitenzi vingi sana vinavyonyambuliwa na kwendeleza mazungumzo ya wazungumzaji.

The content you want is available to Zendy users.

Already have an account? Click here to sign in.
Having issues? You can contact us here